Dr. Slaa Ateuliwa kuwa Katibu Mkuu wa CHADEMA kwa mara nyingine

MWENYEKITI wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema) Taifa,
 Freeman Mbowe amewateua 
Dk. Willbrod Slaa kuwa Katibu Mkuu, John Mnyika kuwa Naibu Katibu Mkuu Bara 
na Salum Mwalim ambaye anakuwa Naibu Katibu Mkuu Zanzibar Viongozi hao 
wameteuliwa jana usiku na kupitishwa na Baraza Kuu la Chadema hivyo 
kufikia tamati ya uchaguzi wa ndani ya chama hicho.Mhe. John Mnyika 
anateuliwa kushika nafasi ambayo ilikuwa inashikiliwa na Mbunge wa Jimbo
 la Kigoma Kaskazini, Mhe. Zitto Kabwe ambaye aliondolewa katika nafasi 
hiyo na kamati kuu ya chama hicho kwa kudaiwa kuvunja katiba ya chama.