Marekani yasema imemuua Ahmed Godane

Taarifa kutoka idara ya ulinzi ya Marekani Pentagon zinasema kuwa mmoja wa wanzilishi wa kundi la Al Shabaab Ahmed Godane ameuawa.
Marekani imesema kuwa kuuawa kwa God
ni hatua kubwa sana katika harakati dhidi ya wapiganaji hao wamekuwa msumari mkali kwa mataifa ya kanda ya Afrika Mashariki na hata kwa serikali ya Somalia yenyewe.
Katibu wa Pentagon Nchini Rear Admiral John Kirby ametangaza kuwa Ahmed Godane ameuawa katika oparesheni iliyofanywa nchini Somalia Jumatatu wiki hii.
Kwa Mujibu wa Admiral Kirby, kuuawa kwa Godane ni pigo kubwa zaidi kwa kundi hilo la Al shabaab na itasaidia kukabiliana na ugaidi unaofanywa na kundi hilo eneo la Afrika Mashariki.
Marekani imekuwa ikishirikiana na washirika wake wakuu kukabili wapiganaji hao wa AL shabaab ambapo katika miaka ya hivi karibuni wamezidisha mashambulio sio tu nchini Somalia bali hadi nchi jirani.
Wiki iliyopita Kikosi cha kulinda amani chini ya mwavuli wa Muungano wa Afrika AMISOM kikishirikiana na majeshi ya serikali ya Somalia kilianzisha oparesheni kali kuwasaka wapiganaji hao wa AL shabaab. Na kufikia mwanzoni mwa wiki hii Marekani ikajiunga katika oparesheni hiyo ambapo walishambulia msafara ambao Ahmed Godane alishukiwa kuwa nda